Biblia Habari Njema

Yohane 10:19-21 Biblia Habari Njema (BHN)

19. Kukawa tena na mafarakano kati ya Wayahudi kwa sababu ya maneno haya.

20. Wengi wao wakasema, “Ana pepo; tena ni mwendawazimu! Ya nini kumsikiliza?”

21. Wengine wakasema, “Haya si maneno ya mwenye pepo. Je, pepo anaweza kuyafumbua macho ya vipofu?”