Biblia Habari Njema

Matendo 7:40-44 Biblia Habari Njema (BHN)

40. Walimwambia Aroni: ‘Tutengenezee miungu itakayotuongoza njiani, maana hatujui yaliyompata huyo Mose aliyetuongoza kutoka Misri!’

41. Hapo ndipo walipojitengenezea sanamu ya ndama, wakaitambikia na kukifanyia sherehe kitu ambacho ni kazi ya mikono yao wenyewe.

42. Lakini Mungu aliondoka kati yao, akawaacha waabudu nyota za anga, kama ilivyoandikwa katika kitabu cha manabii:‘Enyi watu wa Israeli!Si mimi mliyenitolea tambiko na sadakakwa miaka arubaini kule jangwani!

43. Nyinyi mlikibeba kibanda cha mungu Moloki,na sanamu ya nyota ya mungu wenu Refani.Sanamu mlizozifanya ndizo mlizoabudu.Kwa sababu hiyo nitawapeleka mateka mbali kupita Babuloni!’

44. Kule jangwani babu zetu walikuwa na lile hema la maamuzi. Lilitengenezwa kama Mungu alivyomwambia Mose alifanye; nakala kamili ya kile alichooneshwa.