Biblia Habari Njema

Luka 2:16-21 Biblia Habari Njema (BHN)

16. Basi, wakaenda mbio, wakamkuta Maria na Yosefu na yule mtoto mchanga amelazwa horini.

17. Hao wachungaji walipomwona mtoto huyo wakawajulisha wote habari waliyokuwa wamesikia juu yake.

18. Wote waliosikia hayo walishangaa juu ya habari walizoambiwa na wachungaji.

19. Lakini Maria aliyaweka na kuyatafakari mambo hayo yote moyoni mwake.

20. Wale wachungaji walirudi makwao huku wakimtukuza na kumsifu Mungu kwa yote waliyokuwa wamesikia na kuona; yote yalikuwa kama walivyokuwa wameambiwa.

21. Siku nane baadaye, wakati wa kumtahiri mtoto ulipofika, walimpa jina Yesu, jina ambalo alikuwa amepewa na malaika kabla hajachukuliwa mimba.