Biblia Habari Njema

2 Wafalme 10:26-30 Biblia Habari Njema (BHN)

26. na kutoa nguzo takatifu na kuiteketeza kwa moto.

27. Wakaharibu nguzo pamoja na hekalu; wakaligeuza hekalu kuwa choo; na hivyo ndivyo ilivyo mpaka hivi leo.

28. Hivyo ndivyo Yehu alivyofuta ibada za Baali katika Israeli.

29. Lakini alifuata dhambi ya Yeroboamu mwana wa Nebati ya kuwaongoza Waisraeli watende dhambi. Aliweka sanamu za ndama wa dhahabu huko Betheli na Dani.

30. Mwenyezi-Mungu akamwambia Yehu, “Umewatendea wazawa wa Ahabu yale yote niliyotaka uwatendee. Kwa hiyo nimekuahidi kuwa wazawa wako hadi kizazi cha nne watatawala Israeli.”