Biblia Habari Njema

1 Wafalme 22:37-43 Biblia Habari Njema (BHN)

37. Mfalme Ahabu alipofariki maiti yake ilipelekwa Samaria, ikazikwa huko.

38. Gari lake la kukokotwa waliliosha katika bwawa la Samaria, mbwa wakairamba damu yake, nao makahaba wakaoga humo, sawa kabisa na neno alilosema Mwenyezi-Mungu.

39. Matendo mengine ya mfalme Ahabu, jinsi alivyojenga na kupamba nyumba yake kwa pembe, na miji yote aliyojenga, yote yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Nyakati ya Wafalme wa Israeli.

40. Ahabu alipofariki, mwanawe Ahazia alitawala mahali pake.

41. Mnamo mwaka wa nne wa utawala wa mfalme Ahabu wa Israeli, Yehoshafati mwana wa Asa, alianza kutawala Yuda.

42. Yehoshafati alikuwa na umri wa miaka thelathini na mitano alipoanza kutawala. Alitawala kutoka Yerusalemu kwa muda wa miaka ishirini na mitano. Mama yake alikuwa Azuba binti Shilhi.

43. Alitenda mema mbele ya Mwenyezi-Mungu kama alivyofanya baba yake Asa.