10. Basi, wakamwuliza, “Sasa, macho yako yalipataje kufumbuliwa?”
11. Naye akawajibu, “Yule mtu aitwaye Yesu alifanya tope, akanipaka machoni na kuniambia: ‘Nenda ukanawe katika bwawa la Siloamu.’ Hapo, mimi nikaenda, nikanawa, nikapata kuona.”
12. Wakamwuliza, “Yeye yuko wapi?” Naye akawajibu, “Mimi sijui!”