Biblia Habari Njema

Yohane 8:54-59 Biblia Habari Njema (BHN)

54. Yesu akawajibu, “Nikijitukuza mwenyewe, utukufu wangu si kitu. Baba yangu ambaye nyinyi mwasema ni Baba yenu, ndiye anayenitukuza.

55. Nyinyi hamjapata kumjua, lakini mimi namjua. Na, nikisema simjui, nitakuwa mwongo kama nyinyi. Mimi namjua na ninashika neno lake.

56. Abrahamu, baba yenu, alishangilia aione siku yangu; naye aliiona, akafurahi.”

57. Basi, Wayahudi wakamwambia, “Wewe hujatimiza miaka hamsini bado, nawe umemwona Abrahamu?”

58. Yesu akawaambia, “Kweli nawaambieni, kabla Abrahamu hajazaliwa, mimi niko.”

59. Hapo wakaokota mawe ili wamtupie, lakini Yesu akajificha, akatoka hekaluni.