32. Mtaujua ukweli, nao ukweli utawapeni uhuru.”
33. Nao wakamjibu, “Sisi ni wazawa wa Abrahamu, na hatujapata kamwe kuwa watumwa wa mtu yeyote yule. Una maana gani unaposema: ‘Mtakuwa huru?’”
34. Yesu akawajibu, “Kweli nawaambieni, kila mtu anayetenda dhambi ni mtumwa wa dhambi.
35. Mtumwa hana makao ya kudumu nyumbani, lakini mwana anayo makao ya kudumu.