Biblia Habari Njema

Yohane 8:15-20 Biblia Habari Njema (BHN)

15. Nyinyi mnahukumu kwa fikira za kibinadamu, lakini mimi simhukumu mtu.

16. Hata nikihukumu, hukumu yangu ni halali kwa sababu mimi siko peke yangu; Baba aliyenituma yuko pamoja nami.

17. Imeandikwa katika sheria yenu ya kwamba ushahidi wa watu wawili ni halali.

18. Mimi najishuhudia mwenyewe, naye Baba aliyenituma, ananishuhudia pia.”

19. Hapo wakamwuliza, “Baba yako yuko wapi?” Yesu akawajibu, “Nyinyi hamnijui mimi wala hammjui Baba. Kama mngenijua mimi, mngemjua na Baba yangu pia.”

20. Yesu alisema maneno hayo kwenye chumba cha hazina alipokuwa anafundisha hekaluni. Wala hakuna mtu aliyemtia nguvuni, kwa sababu saa yake ilikuwa haijafika bado.