Biblia Habari Njema

Yohane 8:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Lakini Yesu akaenda kwenye mlima wa Mizeituni.

2. Kesho yake asubuhi na mapema alikwenda tena hekaluni. Watu wote wakamwendea, naye akaketi akawa anawafundisha.

3. Basi, waalimu wa sheria na Mafarisayo wakamletea mwanamke mmoja aliyefumaniwa katika uzinzi. Wakamsimamisha katikati yao.

4. Kisha wakamwuliza Yesu, “Mwalimu! Mwanamke huyu alifumaniwa katika uzinzi.