Biblia Habari Njema

Yohane 7:40-45 Biblia Habari Njema (BHN)

40. Baadhi ya watu katika ule umati walisikia maneno hayo, wakasema, “Kweli mtu huyu ndiye yule nabii!”

41. Wengine wakasema, “Huyu ndiye Kristo!” Lakini wengine walisema, “Je, yawezekana Kristo akatoka Galilaya?

42. Maandiko Matakatifu yasemaje? Yanasema: ‘Kristo atatoka katika ukoo wa Daudi, na atazaliwa Bethlehemu, mji wa Daudi!’”

43. Basi, kukatokea mafarakano juu yake katika ule umati wa watu.

44. Baadhi ya watu walitaka kumtia nguvuni lakini hakuna aliyejaribu kumkamata.

45. Kisha wale walinzi wakarudi kwa makuhani wakuu na Mafarisayo; nao wakawauliza, “Kwa nini hamkumleta?”