Biblia Habari Njema

Yohane 6:48-57 Biblia Habari Njema (BHN)

48. Mimi ni mkate wa uhai.

49. Wazee wenu walikula mana kule jangwani, lakini walikufa.

50. Lakini huu ni mkate unaoshuka kutoka mbinguni ili yeyote atakayeula asife.

51. Mimi ni mkate hai ulioshuka kutoka mbinguni. Mtu yeyote akila mkate huu ataishi milele. Na mkate nitakaompa ni mwili wangu ninaoutoa kwa ajili ya uhai wa ulimwengu.”

52. Ndipo Wayahudi wakaanza kubishana kati yao: “Anawezaje huyu kutupa mwili wake, tule?”

53. Yesu akawaambia, “Kweli nawaambieni, msipokula mwili wa Mwana wa Mtu na kunywa damu yake, hamtakuwa na uhai ndani yenu.

54. Anayekula mwili wangu na kunywa damu yangu anao uhai wa milele, nami nitamfufua siku ya mwisho.

55. Maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli.

56. Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu, akaa ndani yangu, nami nakaa ndani yake.

57. Baba aliye hai alinituma, nami naishi kwa sababu yake; vivyo hivyo anilaye mimi ataishi pia kwa sababu yangu.