Biblia Habari Njema

Yohane 6:45-51 Biblia Habari Njema (BHN)

45. Manabii wameandika: ‘Watu wote watafundishwa na Mungu.’ Kila mtu anayemsikia Baba na kujifunza kutoka kwake, huja kwangu.

46. Hii haina maana kwamba yupo mtu aliyemwona Baba, isipokuwa yule aliyetoka kwa Mungu; huyo ndiye aliyemwona Baba.

47. Kweli, nawaambieni, anayeamini anao uhai wa milele.

48. Mimi ni mkate wa uhai.

49. Wazee wenu walikula mana kule jangwani, lakini walikufa.

50. Lakini huu ni mkate unaoshuka kutoka mbinguni ili yeyote atakayeula asife.

51. Mimi ni mkate hai ulioshuka kutoka mbinguni. Mtu yeyote akila mkate huu ataishi milele. Na mkate nitakaompa ni mwili wangu ninaoutoa kwa ajili ya uhai wa ulimwengu.”