Biblia Habari Njema

Yohane 6:45-48 Biblia Habari Njema (BHN)

45. Manabii wameandika: ‘Watu wote watafundishwa na Mungu.’ Kila mtu anayemsikia Baba na kujifunza kutoka kwake, huja kwangu.

46. Hii haina maana kwamba yupo mtu aliyemwona Baba, isipokuwa yule aliyetoka kwa Mungu; huyo ndiye aliyemwona Baba.

47. Kweli, nawaambieni, anayeamini anao uhai wa milele.

48. Mimi ni mkate wa uhai.