Biblia Habari Njema

Yohane 6:35-38 Biblia Habari Njema (BHN)

35. Yesu akawaambia, “Mimi ndimi mkate wa uhai. Anayekuja kwangu hataona njaa; anayeniamini hataona kiu kamwe.

36. Lakini niliwaambieni kwamba ingawa mmeniona hamniamini.

37. Wote anaonipa Baba watakuja kwangu; nami kamwe sitamtupa nje yeyote anayekuja kwangu,

38. kwani nimeshuka kutoka mbinguni si kwa ajili ya kufanya matakwa yangu, ila kutimiza matakwa ya yule aliyenituma.