Biblia Habari Njema

Yohane 4:31-37 Biblia Habari Njema (BHN)

31. Wakati huohuo wanafunzi wake walikuwa wanamsihi Yesu: “Mwalimu, kula chakula.”

32. Lakini Yesu akawaambia, “Mimi ninacho chakula msichokijua nyinyi.”

33. Wanafunzi wake wakaulizana, “Je, kuna mtu aliyemletea chakula?”

34. Yesu akawaambia, “Chakula changu ni kufanya anachotaka yule aliyenituma na kuitimiza kazi yake.

35. Nyinyi mwasema: ‘Bado miezi minne tu, na wakati wa mavuno utafika!’ Lakini mimi nawaambieni, angalieni mkaone jinsi mashamba yalivyo tayari kuvunwa.

36. Mvunaji anapata mshahara wake, na anakusanya mavuno kwa ajili ya uhai wa milele; hivyo mpandaji na mvunaji watafurahi pamoja.

37. Kwa sababu hiyo msemo huu ni kweli: ‘Mmoja hupanda na mwingine huvuna.’