Biblia Habari Njema

Yohane 4:1-6 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Mafarisayo walisikia kwamba Yesu alikuwa anabatiza na kuwapata wanafunzi wengi kuliko Yohane.

2. (Lakini ukweli ni kwamba Yesu hakuwa anabatiza ila wanafunzi wake.)

3. Basi, Yesu aliposikia hayo, alitoka Yudea akarudi Galilaya;

4. na katika safari hiyo ilimbidi apitie Samaria.

5. Basi, akafika Sukari, mji mmoja wa Samaria, karibu na shamba ambalo Yakobo alikuwa amempa mwanawe, Yosefu.

6. Mahali hapo palikuwa na kisima cha Yakobo, naye Yesu, kutokana na uchovu wa safari, akaketi kando ya kisima. Ilikuwa yapata saa sita mchana.