Biblia Habari Njema

Yohane 2:19-21 Biblia Habari Njema (BHN)

19. Yesu akawaambia, “Vunjeni hekalu hili, nami nitalijenga kwa siku tatu.”

20. Hapo Wayahudi wakasema, “Hekalu hili lilijengwa kwa muda wa miaka arubaini na sita. Je, wewe utalijenga kwa siku tatu?”

21. Lakini Yesu alikuwa anaongea juu ya hekalu ambalo ni mwili wake.