Biblia Habari Njema

Yohane 2:1-6 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Siku ya tatu kulikuwa na harusi mjini Kana, mkoani Galilaya. Mama yake Yesu alikuwapo,

2. naye Yesu alikuwa amealikwa harusini pamoja na wanafunzi wake.

3. Divai ilipokwisha, mama yake akamwambia, “Hawana divai!”

4. Yesu akamjibu, “Mama, usiniambie la kufanya. Saa yangu bado.”

5. Hapo mama yake akawaambia watumishi, “Lolote atakalowaambieni, fanyeni.”

6. Hapo palikuwa na mitungi sita ya mawe, ambayo kila mmoja uliweza kuchukua kiasi cha madebe mawili au matatu. Ilikuwa imewekwa hapo kufuatana na desturi ya Kiyahudi ya kutawadha.