Biblia Habari Njema

Yohane 2:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Siku ya tatu kulikuwa na harusi mjini Kana, mkoani Galilaya. Mama yake Yesu alikuwapo,

2. naye Yesu alikuwa amealikwa harusini pamoja na wanafunzi wake.

3. Divai ilipokwisha, mama yake akamwambia, “Hawana divai!”

4. Yesu akamjibu, “Mama, usiniambie la kufanya. Saa yangu bado.”

5. Hapo mama yake akawaambia watumishi, “Lolote atakalowaambieni, fanyeni.”