Biblia Habari Njema

Yohane 16:1-6 Biblia Habari Njema (BHN)

1. “Nimewaambieni hayo kusudi msiiache imani yenu.

2. Watu watawafukuza nyinyi katika masunagogi yao. Tena, wakati unakuja ambapo kila atakayewaua nyinyi atadhani anamhudumia Mungu.

3. Watawatendeeni mambo hayo kwa sababu hawamjui Baba, wala hawanijui mimi.

4. Basi, nimewaambieni mambo haya ili saa yake itakapofika mkumbuke kwamba niliwaambieni.“Sikuwaambieni mambo haya tangu mwanzo kwa sababu nilikuwa pamoja nanyi.

5. Lakini sasa namwendea yule aliyenituma; na hakuna hata mmoja wenu anayeniuliza: ‘Unakwenda wapi?’

6. Kwa kuwa nimewaambieni mambo hayo mmejaa huzuni mioyoni mwenu.