Biblia Habari Njema

Yohane 16:1-3 Biblia Habari Njema (BHN)

1. “Nimewaambieni hayo kusudi msiiache imani yenu.

2. Watu watawafukuza nyinyi katika masunagogi yao. Tena, wakati unakuja ambapo kila atakayewaua nyinyi atadhani anamhudumia Mungu.

3. Watawatendeeni mambo hayo kwa sababu hawamjui Baba, wala hawanijui mimi.