Biblia Habari Njema

Yohane 15:12-16 Biblia Habari Njema (BHN)

12. Hii ndiyo amri yangu: Pendaneni; pendaneni kama nilivyowapenda nyinyi.

13. Hakuna upendo mkuu zaidi kuliko upendo wa mtu atoaye uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.

14. Nyinyi ni rafiki zangu mkifanya ninayowaamuru.

15. Nyinyi siwaiti tena watumishi, maana mtumishi hajui anachofanya bwana wake. Lakini mimi nimewaita nyinyi rafiki, kwa sababu nimewajulisha yote ambayo nimeyasikia kutoka kwa Baba yangu.

16. Nyinyi hamkunichagua mimi; mimi niliwachagueni na kuwatuma mwende mkazae matunda, matunda yadumuyo, naye Baba apate kuwapeni chochote mnachomwomba kwa jina langu.