Biblia Habari Njema

Yohane 14:16-20 Biblia Habari Njema (BHN)

16. Nami nitamwomba Baba naye atawapeni Msaidizi mwingine, atakayekaa nanyi milele.

17. Yeye ni Roho wa ukweli. Ulimwengu hauwezi kumpokea kwa sababu hauwezi kumwona wala kumjua. Lakini nyinyi mnamjua kwa sababu anabaki nanyi na yu ndani yenu.

18. “Sitawaacha nyinyi yatima; nitakuja tena kwenu.

19. Bado kidogo nao ulimwengu hautaniona tena, lakini nyinyi mtaniona; na kwa kuwa mimi ni hai, nanyi pia mtakuwa hai.

20. Siku ile itakapofika mtajua kwamba mimi niko ndani ya Baba, nanyi mko ndani yangu, nami ndani yenu.