Biblia Habari Njema

Yohane 14:14-17 Biblia Habari Njema (BHN)

14. Mkiniomba chochote kwa jina langu, nitawafanyieni.

15. “Mkinipenda mtazishika amri zangu.

16. Nami nitamwomba Baba naye atawapeni Msaidizi mwingine, atakayekaa nanyi milele.

17. Yeye ni Roho wa ukweli. Ulimwengu hauwezi kumpokea kwa sababu hauwezi kumwona wala kumjua. Lakini nyinyi mnamjua kwa sababu anabaki nanyi na yu ndani yenu.