Biblia Habari Njema

Yohane 13:32-35 Biblia Habari Njema (BHN)

32. Na kama utukufu wa Mungu umefunuliwa ndani ya Mwana, basi, naye Mungu ataudhihirisha utukufu wa Mwana ndani yake mwenyewe, na atafanya hivyo mara.

33. “Watoto wangu, bado niko nanyi kwa muda mfupi tu. Mtanitafuta, lakini sasa nawaambieni yale niliyowaambia viongozi wa Wayahudi: ‘Niendako nyinyi hamwezi kwenda!’

34. Nawapeni amri mpya: Pendaneni; pendaneni kama nilivyowapenda nyinyi.

35. Mkipendana, watu wote watajua kwamba nyinyi ni wanafunzi wangu.”