Biblia Habari Njema

Yohane 12:22-25 Biblia Habari Njema (BHN)

22. Filipo akaenda, akamwambia Andrea, nao wawili wakaenda kumwambia Yesu.

23. Yesu akawaambia, “Saa ya kutukuzwa kwa Mwana wa Mtu imefika!

24. Kweli nawaambieni, punje ya ngano hubaki punje tu isipokuwa ikianguka katika udongo na kufa. Kama ikifa, basi huzaa matunda mengi.

25. Anayependa maisha yake, atayapoteza; anayeyachukia maisha yake katika ulimwengu huu, atayaweka kwa ajili ya uhai wa milele.