12. Kesho yake, kundi kubwa la watu waliokuja kwenye sikukuu walisikia kuwa Yesu alikuwa njiani kuja Yerusalemu.
13. Basi, wakachukua matawi ya mitende, wakatoka kwenda kumlaki; wakapaza sauti wakisema:“Sifa! Abarikiwe huyo ajaye kwa jina la Bwana.Abarikiwe mfalme wa Israeli.”
14. Yesu akampata mwanapunda mmoja, akapanda juu yake kama yasemavyo Maandiko:
15. “Usiogope mji wa Siyoni!Tazama, Mfalme wako anakuja,amepanda mwanapunda!”