Biblia Habari Njema

Yohane 11:37-40 Biblia Habari Njema (BHN)

37. Lakini baadhi yao wakasema, “Je, huyu aliyemfumbua macho yule kipofu, hakuweza kumfanya Lazaro asife?”

38. Basi, Yesu akiwa amehuzunika tena moyoni, akafika kaburini. Kaburi lenyewe lilikuwa pango, na lilikuwa limefunikwa kwa jiwe.

39. Yesu akasema, “Ondoeni hilo jiwe!” Martha, dada yake huyo aliyekufa, akamwambia, “Bwana, amekwisha anza kunuka; amekaa kaburini siku nne!”

40. Yesu akamwambia, “Je, sikukuambia kwamba ukiamini utaona utukufu wa Mungu?”