Biblia Habari Njema

Yohane 11:29-35 Biblia Habari Njema (BHN)

29. Naye aliposikia hivyo, akainuka mara, akamwendea Yesu.

30. Yesu alikuwa hajaingia kijijini, ila alikuwa bado mahali palepale Martha alipomlaki.

31. Basi, Wayahudi waliokuwa nyumbani pamoja na Maria wakimfariji walipomwona ameinuka na kutoka nje ghafla, walimfuata. Walidhani alikuwa anakwenda kaburini kuomboleza.

32. Basi, Maria alipofika mahali pale Yesu alipokuwa na kumwona, alipiga magoti, akamwambia, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, kaka yangu hangalikufa!”

33. Yesu alipomwona analia, na wale Wayahudi waliokuja pamoja naye wanalia pia, alijawa na huzuni na kufadhaika moyoni.

34. Kisha akawauliza, “Mlimweka wapi?” Wakamwambia, “Bwana, njoo uone.”

35. Yesu akalia machozi.