Biblia Habari Njema

Yohane 10:5-9 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Kondoo hao hawawezi kumfuata mgeni, bali watamkimbia kwa sababu hawaijui sauti yake.”

6. Yesu aliwaambia mfano huo, lakini wao hawakuelewa alichotaka kuwaambia.

7. Basi, akasema tena, “Kweli nawaambieni, mimi ni mlango wa kondoo.

8. Wale wengine wote waliokuja kabla yangu ni wezi na wanyanganyi, nao kondoo hawakuwasikiliza.

9. Mimi ni mlango. Anayeingia kwa kupitia kwangu ataokolewa; ataingia na kutoka, na kupata malisho.