Biblia Habari Njema

Yohane 10:25-31 Biblia Habari Njema (BHN)

25. Yesu akawajibu, “Nimewaambieni, lakini hamsadiki. Kazi ninazozifanya mimi kwa jina la Baba yangu zinanishuhudia.

26. Lakini nyinyi hamsadiki kwa sababu nyinyi si kondoo wangu.

27. Kondoo wangu huisikia sauti yangu; mimi nawajua, nao hunifuata.

28. Mimi nawapa uhai wa milele; nao hawatapotea milele, wala hakuna mtu atakayeweza kuwatoa mkononi mwangu.

29. Baba yangu ambaye ndiye aliyenipa hao ni mkuu kuliko wote, wala hakuna awezaye kuwatoa mikononi mwake Baba.

30. Mimi na Baba, tu mmoja.”

31. Basi, Wayahudi wakachukua mawe ili wamtupie.