Biblia Habari Njema

Yohane 1:43-45 Biblia Habari Njema (BHN)

43. Kesho yake Yesu aliamua kwenda Galilaya. Basi, akamkuta Filipo, akamwambia, “Nifuate.”

44. Filipo alikuwa mwenyeji wa Bethsaida, mji wa akina Andrea na Petro.

45. Naye Filipo akamkuta Nathanaeli, akamwambia, “Tumemwona yule ambaye Mose aliandika juu yake katika kitabu cha sheria, na ambaye manabii waliandika habari zake, yaani Yesu Mwana wa Yosefu, kutoka Nazareti.”