Biblia Habari Njema

Mhubiri 10:2-9 Biblia Habari Njema (BHN)

2. Moyo wa mwenye hekima humwongoza kutenda yaliyo sawa;lakini mtu mpumbavu moyo wake humpotosha.

3. Hata apitapo njiani, mpumbavu hutambulikana hivyo,humjulisha kila mtu kwamba yeye ni mpumbavu.

4. Mtawala akikuwakia hasira, usijiuzulu;makosa makubwa huweza kufutwa ukiwa mnyenyekevu.

5. Kuna uovu niliogundua hapa duniani, uovu unaosababishwa na watawala:

6. Kwamba wapumbavu wanapewa kazi za madaraka ya juu, na matajiri wanachukua nafasi za mwisho.

7. Nimeona watumwa wanapanda farasi, na wakuu wanatembea kwa miguu kama watumwa.

8. Mchimba shimo hutumbukia mwenyewe,abomoaye ukuta huumwa na nyoka.

9. Mchonga mawe huumizwa nayo,mkata kuni hukabiliwa na hatari.