Biblia Habari Njema

Matendo 5:16-19 Biblia Habari Njema (BHN)

16. Watu wengi walifika kutoka katika miji ya kandokando ya Yerusalemu, wakiwaleta wagonjwa wao na wale waliokuwa na pepo wachafu, nao wote wakaponywa.

17. Kisha, kuhani mkuu na wenzake waliokuwa wa kikundi cha Masadukayo wa mahali hapo, wakawaonea mitume wivu.

18. Basi, wakawatia nguvuni, wakawafunga ndani ya gereza kuu.

19. Lakini usiku malaika wa Bwana aliifungua milango ya gereza, akawatoa nje, akawaambia,