Biblia Habari Njema

Matendo 2:28-32 Biblia Habari Njema (BHN)

28. Umenionesha njia za uhai,umenijaza furaha kwa kuwako kwako!’

29. “Ndugu zangu, napenda kuwaambieni waziwazi juu ya mambo yaliyompata Daudi, babu yetu. Yeye alikufa, akazikwa, tena kaburi lake liko papa hapa petu mpaka leo.

30. Lakini kwa vile Daudi alikuwa nabii, alijua kuwa Mungu alimwapia kiapo kwamba atamtawaza mmoja wa uzawa wake kuwa mfalme mahali pake.

31. Daudi aliona kabla mambo yatakayofanywa na Mungu na hivyo akasema juu ya ufufuo wa Kristo wakati aliposema: ‘Hakuachwa kuzimu, mwili wake haukuoza.’

32. Basi, Mungu alimfufua huyo Yesu na sisi sote ni mashahidi wa tukio hilo.