Biblia Habari Njema

Matendo 19:38-41 Biblia Habari Njema (BHN)

38. Kama, basi Demetrio na wafanyakazi wake wana mashtaka yao kuhusu watu hawa, yapo mahakama na wakuu wa mikoa; wanaweza kushtakiana huko.

39. Kama mna matatizo mengine, yapelekeni katika kikao halali.

40. Kwa maana tungaliweza kushtakiwa kwa kusababisha ghasia kutokana na vituko vya leo. Ghasia hii haina msingi halali na hatungeweza kutoa sababu za kuridhisha za ghasia hiyo.”

41. Baada ya kusema hayo, aliuvunja mkutano.