Biblia Habari Njema

Matendo 17:32-34 Biblia Habari Njema (BHN)

32. Walipomsikia Paulo anasema juu ya jambo la kufufuka kwa wafu, wengine wao waliangua kicheko; lakini wengine walisema, “Tunataka kukusikia tena juu ya jambo hili!”

33. Hivyo, Paulo aliwaacha, akatoka barazani.

34. Lakini watu kadhaa waliandamana naye, wakawa waumini. Miongoni mwao walikuwa Dionisio wa Areopago, na mwanamke mmoja aitwaye Damari na wengineo.