Biblia Habari Njema

Matendo 16:32-34 Biblia Habari Njema (BHN)

32. Basi, wakamhubiria neno la Bwana yeye pamoja na jamaa yake.

33. Yule askari aliwachukua saa ileile ya usiku akawasafisha majeraha yao, kisha yeye na jamaa yake wakabatizwa papo hapo. [

34. Halafu akawachukua Paulo na Sila nyumbani kwake, akawapa chakula. Yeye na jamaa yake yote wakafanya sherehe kwa vile sasa walikuwa wanamwamini Mungu].