Biblia Habari Njema

Matendo 14:18-20 Biblia Habari Njema (BHN)

18. Ingawa walisema hivyo haikuwa rahisi kuwazuia wale watu wasiwatambikie.

19. Lakini Wayahudi kadhaa walikuja kutoka Antiokia na Ikonio, wakawafanya watu wajiunge nao, wakampiga mawe Paulo na kumburuta hadi nje ya mji wakidhani amekwisha kufa.

20. Lakini waumini walipokusanyika na kumzunguka, aliamka, akarudi mjini. Kesho yake, yeye pamoja na Barnaba walikwenda Derbe.