Biblia Habari Njema

Matendo 10:16-21 Biblia Habari Njema (BHN)

16. Jambo hili lilifanyika mara tatu, kisha ile shuka ikarudishwa juu mbinguni.

17. Petro alipokuwa bado anashangaa juu ya maana ya hayo maono aliyokuwa ameyaona, wale watu waliotumwa na Kornelio, baada ya kuigundua nyumba ya Simoni, walifika mlangoni,

18. wakaita kwa sauti: “Je, kuna mgeni humu aitwaye Simoni Petro?”

19. Petro alikuwa bado anajaribu kuelewa yale maono, na hapo Roho akamwambia, “Sikiliza! Kuna watu watatu hapa, wanakutafuta.

20. Shuka upesi na wala usisite kwenda pamoja nao kwa maana ni mimi niliyewatuma.”

21. Basi, Petro akateremka chini, akawaambia hao watu, “Mimi ndiye mnayemtafuta. Kwa nini mmekuja?”