Biblia Habari Njema

Matendo 1:18-20 Biblia Habari Njema (BHN)

18. Yeye alinunua shamba kwa zile fedha alizopata kutokana na kitendo chake kiovu, akaanguka chini, akapasuka na matumbo yake yakamwagika nje.

19. Kila mtu katika Yerusalemu alisikia habari za tukio hilo na hivyo, kwa lugha yao, wakaliita lile shamba “Akel Dama,” maana yake, “Shamba la Damu.”)

20. “Basi, imeandikwa katika kitabu cha Zaburi:‘Makao yake yabaki mahame;mtu yeyote asiishi ndani yake.’Tena imeandikwa:‘Mtu mwingine achukue nafasi yake ya huduma.’