Biblia Habari Njema

Luka 7:14-17 Biblia Habari Njema (BHN)

14. Kisha, akaenda akaligusa lile jeneza, na wale waliokuwa wamelichukua wakasimama. Halafu akasema, “Kijana! Nakuamuru, amka!”

15. Yule aliyekufa akaketi, akaanza kuongea. Na Yesu akamkabidhi kwa mama yake.

16. Watu wote walishikwa na hofu, wakawa wanamtukuza Mungu wakisema, “Nabii mkuu ametokea kati yetu. Mungu amekuja kuwakomboa watu wake.”

17. Habari hizo zikaenea kote katika Yudea na katika nchi za jirani.