Biblia Habari Njema

Luka 7:10-13 Biblia Habari Njema (BHN)

10. Wale watu walipowasili nyumbani walimkuta yule mtumishi hajambo kabisa.

11. Baadaye kidogo, Yesu alikwenda katika mji mmoja uitwao Naini, na wafuasi wake na kundi kubwa la watu waliandamana naye.

12. Basi, alipokuwa anakaribia lango la mji, walitokea watu wamebeba maiti ya mwanamume mmoja, mtoto wa pekee wa mama mjane. Watu wengi wa mji ule walikuwa pamoja na huyo mama.

13. Bwana alipomwona mama huyo akamwonea huruma, akamwambia, “Usilie.”