Biblia Habari Njema

Luka 6:8-13 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Lakini Yesu alijua mawazo yao, akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, “Inuka, simama katikati.” Yule mtu akaenda kusimama katikati.

9. Kisha Yesu akawaambia, “Nawaulizeni, je, ni halali siku ya Sabato kutenda jambo jema au kutenda jambo baya; kuokoa maisha au kuyaangamiza?”

10. Baada ya kuwatazama wote waliokuwa pale, akamwambia yule mtu, “Nyosha mkono wako.” Naye akafanya hivyo, na mkono wake ukawa mzima tena.

11. Lakini wao wakakasirika sana, wakajadiliana jinsi ya kumtendea Yesu maovu.

12. Siku moja Yesu alikwenda mlimani kusali, akakesha huko usiku kucha akisali.

13. Kesho yake aliwaita wanafunzi wake, na miongoni mwao akawachagua watu kumi na wawili ambao aliwaita mitume: