Biblia Habari Njema

Luka 4:6-13 Biblia Habari Njema (BHN)

6. “Nitakupa uwezo juu ya falme zote hizi na fahari zake, kwa maana nimepewa hivi vyote; nikitaka kumpa mtu ninaweza.

7. Hivi vyote vitakuwa mali yako wewe, kama ukiniabudu.”

8. Yesu akamjibu, “Imeandikwa:‘Utamwabudu Bwana Mungu wako,na kumtumikia yeye peke yake.’”

9. Ibilisi akamchukua mpaka Yerusalemu, kwenye mnara wa hekalu, akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, jitupe chini

10. kwa maana imeandikwa:‘Atawaamuru malaika wake wakulinde,’

11. na tena,‘Watakuchukua mikononi mwao,usije ukajikwaa mguu kwenye jiwe.’”

12. Lakini Yesu akamjibu, “Imeandikwa: ‘Usimjaribu Bwana Mungu wako.’”

13. Ibilisi alipokwisha mjaribu kwa kila njia, akamwacha kwa muda.