Biblia Habari Njema

Luka 4:19-24 Biblia Habari Njema (BHN)

19. na kutangaza mwaka wa neema ya Bwana.”

20. Baada ya kusoma, akafunga kile kitabu, akampa mtumishi, kisha akaketi; watu wote wakamkodolea macho.

21. Naye akaanza kuwaambia, “Andiko hili mlilosikia limetimia leo.”

22. Wote wakavutiwa sana naye, wakastaajabia maneno mazuri aliyosema. Wakasema, “Je, huyu si mwana wa Yosefu?”

23. Naye akawaambia, “Bila shaka mtaniambia msemo huu: ‘Mganga jiponye mwenyewe,’ na pia mtasema: ‘Yote tuliyosikia umeyafanya kule Kafarnaumu, yafanye pia hapa kijijini mwako.’”

24. Akaendelea kusema, “Hakika nawaambieni, nabii hatambuliwi kijijini mwake.