Biblia Habari Njema

Luka 24:34-40 Biblia Habari Njema (BHN)

34. wakisema, “Hakika Bwana amefufuka, amemtokea Simoni.”

35. Basi, hao wafuasi wawili wakawajulisha yale yaliyowapata njiani, na jinsi walivyomtambua katika kumega mkate.

36. Walipokuwa wakiwaambia hayo, Yesu mwenyewe akasimama kati yao, akawaambia “Amani iwe nanyi.”

37. Wakashtuka na kushikwa na hofu wakidhani wameona mzimu.

38. Lakini yeye akawaambia, “Kwa nini mnafadhaika? Mbona mnakuwa na mashaka mioyoni mwenu?

39. Angalieni mikono na miguu yangu, ya kwamba ni mimi mwenyewe. Nipapaseni mkaone, maana mzimu hauna mwili na mifupa kama mnionavyo.”

40. Baada ya kusema hayo, akawaonesha mikono na miguu.