Biblia Habari Njema

Luka 24:29-32 Biblia Habari Njema (BHN)

29. lakini wao wakamsihi wakisema, “Kaa pamoja nasi, maana kunakuchwa, na usiku unakaribia.” Basi, akaingia kijijini, akakaa pamoja nao.

30. Alipoketi kula chakula pamoja nao, akachukua mkate, akaubariki, akaumega, akawapa.

31. Mara macho yao yakafumbuliwa, wakamtambua; lakini yeye akatoweka kati yao.

32. Basi, wakaambiana, “Je, mioyo yetu haikuwa inawaka ndani yetu wakati alipokuwa anatufafanulia Maandiko Matakatifu kule njiani?”