Biblia Habari Njema

Luka 20:5-8 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Lakini wao wakajadiliana hivi: “Tukisema yalitoka kwa Mungu, yeye atatuuliza: ‘Mbona hamkumsadiki?’

6. Na tukisema yalitoka kwa binadamu, watu wote hapa watatupiga mawe, maana wote wanaamini kwamba Yohane alikuwa nabii.”

7. Basi, wakamwambia, “Hatujui mamlaka hayo yalitoka wapi.”

8. Yesu akawaambia, “Hata mimi sitawaambia ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani.”